Tuesday, May 7, 2019

Marekani kupeleka ndege za kivita 4B-52 Mashariki ya Kati.

Katika harakati za kujiweka imara kiulinzi, Marekani inapangakupeleka ndege za  kivita aina 4B-52, huko Mashariki ya Kati, kitendo kinacho sadikiwa kuwa ni kujitaadhari na mashambulizi toka Iran.

Habari kutoka Pentagon- makao makuu ya usalama wa Marekani, zinasema ndege hizo zipo tiyari kuondoka kuelekea nchi Katar muda wowote wiki hii.


Akiongea kuhusu kupelekwa kwa ndege hizo, mshauri wa masuala ya kiulinzi na usalama wa Marekani, John Bolton amesema, " Marekani imefanya uamuzi huo kutokana na uhalisia wa hali iliyopo katika eneo hilo, na hasa Iran kuonyesha dalili za kujiandaa kivita."

Ndege hizo za kivita zitaondoka katika kutuo cha kijeshi cha ndege kilichopo Louisian nchini Marekani.
Kupangwa kuondoka kwa ndege hizo, kunakuja baada ya melikebu ya kivita ya Makereni kwa jina Abraham Lincoln kuondoka hivi karibuni kuelekea kwenye bahari iliyopo Mashariki ya Kati.

No comments:

Post a Comment