Wednesday, May 8, 2019

Visu vyatishia maisha ya watu jijini London

Matumizi ya visu kudhuru watu katika jiji la London waongezeka.

Ripoti ya Polisi kuhusu matumizi ya visu kama nyenzo ya kudhuria watu yamekuwa makubwa nchi Uingereza tangu mwaka 1946, na Jiji la London  linaongoza kwa matumizi ya visu kama siraha na tangu mwaka uanze wa 2019 hadi kufikia tarehe 27 April, 2019, watu wapatao 27 walipoteza maisha.

Kwa mujibu wa  ripoti, Jiji la London, limekuwa likiongoza katika matumizi ya visu kudhuru watu na kati ya watu 100,000 katika mwaka 2017-18, watu 168 walichomwa na visu na kupoteza maisha.



Ongezeko la matumizi ya visu limeongezeka katika kipindi cha miezi 12 iliyopita ambayo imeishia mwezi wa Septemba 2018, kwa kesi zinazohusha matumizi ya visu kuwa 39,818.

Kwa mujibu wa ripoti ya Polisi, wengi waanaodhurika na kuhusika na matumizi ya visu ni vijana wa Kiafrika na wenye asili ya Kiashia ambao ongezeko lao limefikia 25% kitaifa.


Akiongela kuhusu suala zima la matumizi ya visu kama siraha jijini,  mkuu wa Jeshi la Polisi London Cressida Dick amesema " jeshi la polisi linafanya kila  jitihada kupambana na hali hii ya matumizi ya visu katika jiji la London."

Hata hivyo suala la polisi kupambana na matumizi ya visu limekuwa likikutwa na vikwazo vya kisiasa kwa madai polisi wanachagua watu wasio wazungu kuwakagua na kuwaacha wazungu.


Rais wa Iran atangaza kuwa nchi yake kuendelea kuzalisha virutubisho ya Nuklia.

Rais wa Iran, Hassan Rouhania ametangaza kuwa Iran itaanza kuzalisha virutubisho ninavyo zalisha Nuklia, ikiwa nchi za jumuya ya Ulaya hazitaeleza msimamo wao juu ya suala hilo.

Akitangaza kwa Taifa la Iran, rais Rouhania alisema, Iran itasimamisha mikataba yote iliyo sainiwa kati ya Iran na nchi za EU, ikiwa  urahisi wa vikwazo vya kiuchumi zidi ya Iran utaondolewa kama "Marekani inavyotaka."

Mkataba wa kurahisisha vikwazo kwa Iran,  ulisainiwa miaka minne iliyo pita na unajulikana kama P5+1
Joint Comprehensive Plan of Action ambao (JCPOA) na nchi zilizo shiriki ni  Marekani Uingereza, France, China, Urussi, Ujerumani and Umoja wa Ulaya.


Mbunge wa Marekani aumana vichwa na serikali kuhusu Venezuela.

Ilhan Omar, Mbunge wa Kongresi wa chama cha Demokrati nchini Marekani, amepingana vikali na makamu wa rais Mike Pence kuhusu hali ilivyo Venezuela na ushiriki wa Marekani katika nchi hiyo.

Akiongea Makamu wa Rais Pence amesema, Ilhan ni muumini wa ujamaa"anaye pingana na demokrasia na uhuru wa watu kutaka mabadiriko." Naye Ilhan Omar ambaye ni mbuge kutoka chama cha Demokratiki amesema,  imekuwa ni kawaida "mtu akipinga vitendo visivyo halali vinavyo fanywa na Marekani kuitwa "mpinzani wa demokrasi." Na ukweli ulijieleza wakati wa "vita vya Irak" aliongezea  Ilhan.

Mvutano huu, umekuja baada ya serikali ya Marekani inayo ongozwa na rais Trump na cham cha Republikani kutamka kuwa kinamuunga mkono Juan Guaido, mpizani wa serikali ya Venezulea, na ambaye alijitangazia urais na pia kushutumiwa kwa kuongoza mapindizi ya kijeshi zidi serikali hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment